Baba Yetu
Baba yetu uliye mbinguni, jina lako litukuzwe, ufalme wako uje, mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni. Utupe leo mkate wetu wa kila siku, utusamehe makosa yetu, kama nasi tunavyowasamehe waliotukosea. Usitutie majaribuni, lakini utuokoe maovuni. Amina.
Salamu Maria
Salamu Maria, umejaa neema, Bwana yu nawe. Umebarikiwa kuliko wanawake wote, na Yesu, mzao wa tumbo lako, amebarikiwa. Maria Mtakatifu, Mama wa Mungu, utuombee sisi wenye dhambi, sasa na saa ya kufa kwetu. Amina.
Atukuzwe
Atukuzwe Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu. Kama ilivyokuwa mwanzo, sasa, na siku zote, hata milele na milele. Amina.