Dhamira Yetu
Tunaamini kwamba kila Mkatoliki anastahili kupata mafundisho ya Kanisa, sala, na masomo ya kila siku katika lugha yake mwenyewe. Mkatoliki Kiganjani ni jukwaa la kidigitali linalokusanya rasilimali hizi mahali pamoja, ili imani iwe karibu na wewe — kiganjani mwako.
Tunalofanya
Tunatoa masomo ya kila siku ya liturujia, kitabu kamili cha sala, mafundisho ya Katekismo, na kalenda ya mwaka wa kiliturujia. Yote katika Kiswahili sanifu na rahisi kueleweka.
Imani Yetu
Tunaamini katika Mungu mmoja, Baba mwenyezi, na Yesu Kristo Mwana wake, na Roho Mtakatifu. Tunafundisha kwa uaminifu na Magisterium ya Kanisa Katoliki la Roma.